HABARI MPYA
blink
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo News in picture. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo News in picture. Onyesha machapisho yote

HOJA YA MUUNGANO NA IDADI YA SERIKALI TANZANIA

Written By Unknown on Jumanne, 15 Aprili 2014 | 13:22


Je! marumbano yanayoendelea Bungeni ya juu ya mfumo wa Muungano na idadi ya serikali yanalenga kuwezesha vyama vya upinzani kushinda na kutawala Tanganyika?

Na je Bunge kutekwa na Muungano na idadi ya serikali, Je rasimu ya pili ya Katiba haina hoja nyingine zaidi ya hizo?

Tafadhari piga kura yako, chagua jibu upendalo katika hukurasa huu sehemu ya chini kulia

TUNATOA POLE KWA WATANZANIA KWA KIFO CHA MZEE NGURUMO

Written By Unknown on Jumatatu, 14 Aprili 2014 | 09:28

kwigizenews
Mzee Ngurumo enzi za uhai wake akipokea ufuguo wa Gari kutoka kwa Manamuziki Diamond mara alipotangaza kustaafu muziki na kuhitaji misaada kutoka kwa waungwana ili kumudu maisha.

KWIGIZE NEWS .COM Tunatoa pole kwa wanafamilia ya mwanamuziki nguli wa Tanzania marehemu Mzee Maalim Ngurumo kilichotokea jana katika Hospitali ya Taifa mhimbili alikokuwa amelazwa. kwa kumuenzi blog yetu imeweka wimbo (mtanikumbuka) ambao waliutunga na kuimba pamoja na Marehemu TX Moshi, hii ni moja ya kutoa pole kwa Watanzania. bonyeza hapa kutazama video

ZITTO KABWE ASISITIZA HANG'OKI CHADEMA, ASHUTUMU SLAA NA MBOWE KWA UBABAISHAJI

Written By Unknown on Jumapili, 22 Desemba 2013 | 09:16

Sehemu ya wananchi wa mjini Kasulu waliojitokeza kusikiliza hotuba ya zito kabwe ambayo sehemu kubwa ilihusu kupinga kuvuliwa madaraka ndani ya chama chake pamoja na kuwataka wananchi kuungana kuwapinga viongozi wa Kamati kuu ya CHADEMA iliyowavua uongozi Zitto Kabwe, Dr. Kitilya Mkumbo na Migamba kwa tuhuma za Uhaini na usaliti kwa chama hicho
ZITTO KABWE aliyekuwa Naibu Katibu mkuu na naibu msemaji wa Kambi ya Uoinzani Bungeni (aliyevaa nguo za asili) Muda mfupi baada ya kuvalishwa mavani ya kitemi na wazee wa Heru juu katika JImbo la Kasulu Mjini, kabla ya kuanza kuwahutubia maelfu waliofurika uwanjani hapo. Mkutano huo uliandaliwa na kundi la viongozi wa CHADEMA jimbo ambao pia hivi karibuni wamefukuzwa uongozi na chama hicho ngazi ya wailaya kwa kile kinachotajwa kuwa ni kumuunga mkono ZItto na kupinga uamuzi wa kamati kuu

Viongozi wa Chadema kadhaa hasa wa ngazi za juu wilaya ya Kasulu hawakujitokeza katika mkutano huo.
Maelfu ya wakazi wa Mji wa Kasulu mkoani Kigoma wakimsikiliza mbunge wa Kigoma Kaskazini (aliyefukuzwa unaibu katibu mkuu wa Chadema) wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja ambapo Dr. Slaa alishambuliwa na wananchi wanaopinga kamati kuu ya chama hicho kumfykuza uongozi ZITTO


MEDIA COUNCIL SEASON GREETINGS TO ALL M C T MEMBERS

Written By Unknown on Jumatano, 18 Desemba 2013 | 01:56


IJUE AZAM TV, INAYOTOA HUDUMA YA KISASA NA KUMUWEZESHA MTUMIAJI KUREKODI MATANGAZO

Written By Unknown on Jumanne, 17 Desemba 2013 | 05:59

Kulia katika picha ni Rhys Torrington: Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media Ltd
Habari zimeandikwa na Khadija Mahamba na Lucy Ngongoseke
Dar es Salaam

Huduma za matangazo ya AzamTV zilianza kupatikana hewani Kuanzia Ijumaa Desemba 6, 2013 kwa kuwawezesha wateja waliounganishwa kwenya kisimbuzi kungalia bure hadi hii leo ambapo huduma kwa malipo inaanza rasmi kwa ada ya shilingi 12,500 kwa mwezi.

Kwa kuanzia huduma ya AzamTV itahusisha chaneli 50 zinazojumuisha chaneli maarufu za kimataifa, chaneli maarufu za ndani na chaneli tatu maalumu za Azam ambazo ni:
·         Azam One – burudani kwa familia kutoka Afrika, sehemu kubwa ya matangazo   itakuwa kwa lugha ya Kiswahili.
·         Azam Two – vipindi maalum kutoka sehemu mbalimbali za dunia 
·         SinemaZetu – Chaneli maalumu kwa tamthilia za kitanzania kwa saa 24.
Kwa pamoja, chaneli tajwa zitawapa wateja wigo mpana wa kufaidi matangazo bora ya michezo, tamthilia, watoto na maisha.

Kundi la T-Afica likituwa burudani wakati wa ufunguzi wa ofisi ya AZAMTV siku ya jumatatu tarehe 16 Desemba 2013
Ofisi ilifunguliwa rasmi na Bw. Yusuf Bakhresa: Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media Ltd.

“Ofisi hii ya makao makuu ambayo kwa hakika ni ya kuvutia ni kielelezo cha nia thabiti ya Azam Media kufanya kazi kwa umakini katika shughuli ya utangazaji hapa Tanzania. Dira yetu ni kutoa burudani ya kiwango cha juu kwa familia kwa bei nafuu kote nchini, na baadaye kote barani Afrika. Hili ni jambo ambalo kila mmoja hapa nchini anapaswa kujivunia.” Alisema Bakhresa

Rhys Torrington: Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media Ltd alisema: “Naona faraja kubwa kwamba leo hii AzamTV  ipo sokoni kwa ajili ya kila mtanzania. Tutahabarisha, kuelimisha na zaidi ya yote tutaburudusha watu kote nchini. Huduma yetu inapatikana kwa watu wote – situ katika ofisi hizi lakini pia kupitia mtandao wetu unaohusisha zaidi ya mawakala 50 katika kila mkoa. AzamTV ni ya kudumu”

Azam Media pia inawekeza katika utayarishaji wa vipindi vipya kupitia kampuni yake tanzu, Uhai Productions, kwa kushirikiana na watayarishaji wa vipindi wa hapa Tanzania.

Azam Media Ltd. Ni kampuni tanzu ya kundi la makampuni ya Salim Said Bakhressa (SSB).

Azam TV, ni warushaji wa matangazo ya satelaiti kwa mfumo wa digiti ambayo itawapatia wateja wake burudani ya kiwango cha juu kwa familia kwa bei moja nafuu. Makao Makuu yapo Dar es Salaam, Tanzania amabako ilianzishwa mwaka 2013 malengo yakiwa kusambaa katika  nchi nyingine za Afrika hapo baadaye.

Dira ni kuwa na vipindi tofauti vya kimataifa na pia vya ndani ya nchi  vifaavyo kwa familia, wapenzi wa michezo na watanzania wote wa rika mbalimbali.


Watazamaji wanaweza pia kurekodi wakati wa kuangalia kwa kutumia USB. Ni utaratibu wa kawaida kwamba kisimbuzi kinakuja  na na sehemu ya kuunganisha kwa mfumo wa HDMI ili kupokea  picha ang’avu kwenye luninga.

MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA WATOA MSAADA

Written By Unknown on Alhamisi, 21 Novemba 2013 | 05:13


Bi, Lydia Choma Mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa NHIF akikabidhi msaada wa mashuka kwa mkuu wa Mkoa wa Manyara ili zitumike katika vituo mbalimbali vya utoaji wa huduma za afya Mkoani Manyara

Msaada kama huo umetolewa hivi karibuni baada ya kongamano kama hilo kufanyika mkoani Singida, Dodoma, Tanga na Manyara

DEVELOPMENT CHANGE AND VIEWS IN KIGOMA TOWN


As we know Kigoma is one of Tanzania regions which are getting development slowly, but nowadays there are lot of changes, these changes are in Mind and environmentally, for those who went to Kigoma long time ago definitely you will be surprised to observe changes 

Let us go through below pictures


NHC BUILDING IN KIGOMA TOWN
Moja ya majengo ya Shirika la Nyumba Tanzania, jengo hili linatumiwa na taasisi na mashirika mbalimbali ikiwemo Benki ya CRDB

KIGOMA RAILWAY ROAD TO UJIJI
Barabara kuu ya Kigoma -Ujiji , kushoto ni nyumba za makazi na biashara, miongoni mwa nyumba hizo ni za shirika la nyumba na nyingine ni za watu binafsi

TANZANIA REVENUE AUTHORITY, REGIONAL OFFICE
Jengo la mamlaka ya Mapato TRA mkoa wa Kigoma

KIGOMA TOWN BUS TERMINAL
Kituo cha Daladala Kigoma mjini, ni kituo cha Kisasa na cha Kipekee ambapo abiria kutoka Pande zote za Mji wa Kigoma hupata usafiri wa kwenda maeneo mbalimbali ndani ya manspaa ya Kigoma Ujiji


KIGOMA RAILWAY STATION aka Mwanzo wa Reli


TANZANIA POSTAL BANK IN KIGOMA, IN TRA HOUSE

KIGOMA KAMA SHANGHAI CHINA

Written By Unknown on Jumatano, 20 Novemba 2013 | 00:20


Hii ni sehemu ndogo ya kitega uchumi katika fukwe za ziwa Tanganyika mkoani Kigoma, madhari na sura ya eneo hili hufananishwa na baadhi ya miji na vitega uchumi vilivyoko nchini China

Hata hivyo wakati kukiwa na vitega uchumi, na vyanzo vingi vya kuwezesha kuinua pato la mwanaKigoma, Bado wakazi wenyewe wa Kigoma hawajajitokeza kutumia rasilimali zao kupambana na Maradhi, Ujinga na Umasikini

Utegemeza wa ajira za Umma, bado ni ugonjwa mbaya ambao unalitafuna kundi kubwa la vijana ambao wanaposoma huwaza ajira za serikali au mashirika pekee badala ya kufikiri kujiajiri na kutumia rasilimali zinazowazunguka

Kigoma ni moja ya mikoa yenye fursa nyingi, lakini mtazamo wa kijamii, kisera na kijiografia vimekuwa kikwazo kwa maendeleo ya mkoa huo ambao unazungukwa na misitu ya asili yenye rutuba, hifadhi ya wanyama pori, ndege na vipepeo adimu duniani

Aidha Kigoma pia ni mkoa wenye uasili wa Tanganyika kwa maana ya uwepo wa ziwa lenye kina kirefu duniani na samaki aina ya Migebuka, Ngege, Nyika pamoja na sato, Kigoma pia wanapatikana binadamu wa kale (sokwe) wanaofanana na binadamu kwa asilimia Kubwa

Ili Kigoma iendelee ni lazima wakazi na wazawa wa Kigoma wenyewe wabadili mtazamo na namna ya maisha ili hatimae wabaini, waone na watumie rasilimali hizo kwa ajilli ya maendeleo yao na taifa, lakini pia ni lazima serikali nayo itambue kuwa kama mikoa yenye fursa za kiuchumi haitafunguliwa kwa kuwekewa miundombinu bado hatuukomoi mkoa bali Taifa litaendelea kukosa mapato ya nje .

BIMA YA AFYA YAOMBWA MKOPOWA SH. 500 MILIONI HOSPITALI YA RUFAA SINGIDA

Written By Unknown on Alhamisi, 14 Novemba 2013 | 22:32

Picha inaonesha mojawapo ya majengo ya hospitali ya Rufaa Singida ambayo inatarajwa kuwa ya kipekee katika eneo la kanda ya Kati, Hospitali hii inahitaji mkopo wa sh. 500 milioni kwa ajili ya vifaa tiba ili ianze mwakani

Na. Prosper Kwigize

Mkoa wa Singida umetuma maombi ya mkopo wa vifaa tiba wenye thamani ya sh. Milioni 500 ili kuwezesha kuanza kwa hospitali ya rufaa nayojengwa mkoani humo kwa lengo la kupunguza adha ya wananchi kwenda katika hospitari za Bugando, KCMC na Mhimbili

Akihutubia katika kongamano la mfuko wa taifa wa bima ya afya linalofanyika mkoani Singida kujadili changamoto na mafanikio ya mfuko huo kwa mkoa wa Singida, mkuu wa mkoa wa Sigida Dr. Parseko Kone amesema pesa hizo zitawezesha hospitali hiyo kuanza kabla ya decemba mwaka huu

Dr. kone ametoa rai kwa mjumbe wa bodo ya NHIF taifa Bi. Lyida Choma kuyasimamia maombi hayo ili hospitali hiyo ya rufaa ipate vifaa tiba na kuanza kuhudumia wanachama wa mifuko ya afya kupata matibabu bora kulingana na michango yao

Wakati huo huo, mfuko wa taifa wa bima wa afya NHIF na mfuko wa afya ya jamii CHF umetoa mashuska 170 kwa vituo mbalimbali vya afya na hospitali ya mkoa wa Singida ili kupungiza adha ya mashuka kwa wagonja wanaolazwa
Akikabidhi msaada huo kwa mkuu wa mkoa wa Singida, mjumbe wa Bodi ya NHIF Bi. Lydia Choma amesema hospitali zilizopata uhisani huo ni pamoja na hospitali ya mkoa, hospitali za wilaya za Iramba, Manyoni, pamoja na vituo biafsi.

Ends.

KONGAMANO LA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA SINGIDA

Pichani ni Jengo la Halmashauri ya wilaya ya Iramba mkoani Singida, Iramba inasifika kwa kuw ana mikakati mahili ya kuboresha afya za wananchi kupitia katka kuchangia mfuko wa afya ya jamii CHF

Na. Prosper Kwigize

Halmashauri ya wilaya ya Iramba imepongezwa kwa kuwa ya kwanza kitaifa katika ukusanyaji wa michango na idadi ya wananchama nchini

Hayo yamebainishwa na mkurugenzi wa takwimu na uhai wa bima ya afya taifa Bw. Michael Mhando wakati akitoa maelezo ya hali ya mfuko wa taifa wa bima ya afya katika kongamano linalofanyika mkoani Singida kujadili maendeleo ya mfuko huo

Bw. Mhando amebainisha kuwa hadi june mwaka huu mkoa wa Singida umesajili wanachama wachangiaji 12,537 na idadi ya wanaonufaika ni 68, 210

Aidha amewataka waajili wote kuhakikisha wanawahamasisha watumishi wao kujiunga na kuchangia mfuko wa bima ya afya na mfuko wa afya ya jamii ili kuondokana na changamoto za kupata matibabu wanapougua.
Mkuu wa mkoa wa Singida Dr. Parseko Kone amesema viongozi wengi hawajatimiza wajibu wao wa kuwahamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii CHF mkoani Singida

Dr. Kone amebainisha kuwa katika kipindi cha January hadi septemba 30 mwaka huu jumla ya kaya 45,575 kati ya 259251 sawa na asilimia 17.6% wamejiunga ma mfuko wa afya ya jamii mkoani Singida

Kutokana na idadi ndogo ya wanachama Mkuu huyo wa mkoa ameagiza wakuu wa wilaya zote za mkoa wa Singida kuhakikisha wanapatia taarifa kila baada ya miezi miwili ikionesha ni wanachama wangapi wapya wamejiunga na mfuko huo wa afya ya jamii CHF

Aidha Dr. Kone amemuagiza mganga wa mkoa Dr. Doroth kuhakikisha anaitisha kikao cha waganga wote wa wilaya kabla ya tarehe 30 mwezi huu ili kujadili na kuamua namna bora ya kuandikisha wanachama wapya na utoaji wa huduma bora kwa wanachama

Ameonya pia tabia ya waganga kutowathamini wanachama katika kuwapa huduma na kujali wanaolipa esa tasilimu dirishani na kusisitiza kuwa kitendoo hicho kina tafsiri ya ufisadi kwa pesa zinazolipwa na wasio wanachama wa mifuko ya afya ya jamii


Kufuatia hali hiyo Dr. Kone ametoa wito kwa wanachama watakaobaguliwa katika vituo vya afya na hospitali pindi wanapohitaji matibabu kutoa taarifa kwa kiongozi yeyote wa serikali ili madaktari hao wachukuliwe hatua 

FREEDOM OF PRESS IN TANZANIA AND PEACE IN DENGER ZONE

Written By Unknown on Jumanne, 9 Julai 2013 | 10:59




 


Tanzania is blessed country due to so many aspect compare to many African countries as well as western, Asia and American countries, journalists is one of professional group who being used to announce this story over the world, but their now hunted innocently


Sometimes Tanzania it’s called Peace Island in the world, this name came because of Tanzanian life style, hospitality, political and security situation, natural wealth especially forest, hills, mountain, minerals water and land



In few days ago Tanzania has observed lot of criminal events that shows that our good image is going to be changed from Peace Island to country of conflict



I believe that everyone know what is happen in Iringa last year, whereby one Journalist late Mwangosi were killed when he was in his duty of making Political coverage, we know what was happen too Mr. Kibanda the Editors Forum Chairman



Either we know also what happened In Mtwara, whereby journalist were hunted by civilians who managed also to burnt journalist houses , this is aspect show that now Tanzania has forgetern where we come from, where we are and where we want to go



Let us see in picture what Media Council of Tanzania decided was, to prevent ournalists at Job, in above Picture is Journalist at work, while below are one of Mtwara journalist granted a jacket which will be used by them to address the Mtwara community to understand that journalist is friend to them and ignore the perceptions of treating them as enemy  

 



 

 



Either below are picture show the Media council of Tanzania inauguration the book of journalism curriculum, this book will be used by media institution and journalism schools to teach journalist  

 

 
Shukrani kwa : Harold Dickson | Prosper Kwigize | 0752490120
Copyright © 2013. KWIGIZE NEWS AND COMMUNICATION - Haki zote zimeifadhiwa
Email us: kwigizenews@gmail.com
0764243377